• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Mbeya District Council
Mbeya District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya Mbeya

  • Nyumbani
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mifugo na uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi
      • Ufugaji wa nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Wataalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
      • Taarifa ya fedha
      • Mpango wa Mapato na Matumizi
      • Mapato na Matumizi ya Mwezi
      • Taarifa ya miradi ya maendeleo
      • Taarifa ya fedha ya mwaka
      • Mihtasari ya Mikutano ya Baraza
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
      • Mwongozo wa Matumizi ya Vifaa vya TEHAMA
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Picha mwendo
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Kingozi wa Mbizo za Mwenge wa Uhuru 2018 amekabidhi mkopo wa milioni 105

Imewekwa: May 21st, 2018

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2018, Ndg. Charles Kabeho amekabidhi mkopo wa shilingi milioni 105 kwa vikundi 18 vya wanawake vilivyopata shilingi milioni 49 na vikundi vya vijana 9 vilivyopata shilingi milioni 56. Kabeho amekabidhi mkopo huo wakati Mwenge wa Uhuru ulipoenda kukagua shughuli za kikundi cha vijana wafugaji wa kuku “COFAPS”

Akikabidhi mkopo huo Kabeho, ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kwa kutekeleza kwa vitendo sera ya kuwawezesha wananchi kiuchumi ya mwaka 2004 inayoelekeza halmashauri zote nchini kutenga asilimia kumi ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake na vijana.

“Niipongeze Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kwa kuweza kutenga asilimia kumi ya mapato yake kwa ajili ya kuweza kuvikopesha vikundi”

Aidha kabla ya kukabidhi mikopo hiyo, Kabeho alifanya zoezi la kuvihakiki vikundi vyote 27 vilivyopangwa kupatiwa mikopo. Katika ukaguzi huo vikundi 16, vikiwemo vya wanawake 13 na vijana 3 vilikaguliwa na kukabidhiwa hati za mikopo. Vikundi 11 vikiwemo vya wanawake 5 na vijana 6 havikuweza kukaguliwa kwa sababu mbalimmbali zikiwemo kutofika kwa wakati katika eneo la tukio. Na sababu nyingine ni wanavikundi kufika wachache badala ya kufika wote kama alivyoagiza kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2018.

kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2018, Ndg. Charles kabeho akikagua kitambulisho kimojawapo cha wanakikundi cha vijana kabla hajatoa mkopo kwa vijana hao

Kwa vikundi ambavyo hakuvikaguliwa, Kabaho amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, kuvihakiki kama vinasifa ya kupatiwa mkopo, na akikuta kikundi ambacho hakina sifa, fedha zote zirudishwe halmashauri kwa ajili ya kukopesha vikundi vingine vyenye sifa.

Akipokea agizo hilo Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Mhe. Paul Ntinika amesema kwamba atavikagua vikundi hivyo ndani ya siku 5 kwa kushirikiana na kamati yake ya ulinzi na usalama ya wilaya. baada ya kuvikagua atawasilisha taarifa kwa maandishi kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2018 ili aweze kuzifikisha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dakt. John Pombe Magufuli.

Awali akisoma taarifa ya mikopo kwa vikundi vya wanawake na vijana Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Afisa Maendeleo Wilaya, Zena Kapama amesema kwamba halmashauri imejiwekea mkakati wa kutoa mikopo hiyo kila robo, tofauti na hapo awali ambapo ilikua inatoa kwa mkupuo.

Amesema mkopo uliokabidhiwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa vikundi 16 ni wa robo ya nne kwa mwaka wa fedha 2018/2019. Amesema mpaka sasa halmashauri imetoa jumla ya shilingi milioni 435 kwa vikundi 135 vya wanawake na vijana.

Matangazo

  • VITUO VYA KUJIANDIKISHIA ORODHA YA WAPIGA KURA October 11, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA KUJITOLEA KWA KAZI YA MSAIDIZI WA WATOTO MAHAKAMANI February 02, 2022
  • TANGAZO LA ZOEZI LA UTOAJI WA ANWANIZA MAKAZI March 04, 2022
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA March 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • KIAPO CHA UTII KWA WAUGUZI MBEYADC

    May 16, 2025
  • BI. ERICA AMEMTEMBELEA ASKALI ALIELAZWA HOSPITALI YA IFISI

    May 08, 2025
  • Mapokezi ya Mhe Mchengerwa MbeyaDc

    April 26, 2025
  • Karibu Mhe. Mchengerwa

    April 25, 2025
  • Tazama zote

Picha Mwendo

"Wapo Wakuu wa Idara na Vitengo wakiamishwa watu wanafanya sherere" Waitara Naibu waziri TAMISEMI
Picha mwendo zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MBEYA

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti ya mkoa wa Mbeya

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Mahali

Wasiliana nasi

    Mbaliz Road

    Sanduku la posta: 599

    Simu ya mezani: 025-2502260

    Simu ya mkononi: 0762210758

    Baruapepe: ded@mbeyadc.go.tz/info@mbeyadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma zetu

Copyright ©2018 Mbeya District Coucil . All rights reserved.