• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Mbeya District Council
Mbeya District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya Mbeya

  • Nyumbani
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mifugo na uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi
      • Ufugaji wa nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Wataalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
      • Taarifa ya fedha
      • Mpango wa Mapato na Matumizi
      • Mapato na Matumizi ya Mwezi
      • Taarifa ya miradi ya maendeleo
      • Taarifa ya fedha ya mwaka
      • Mihtasari ya Mikutano ya Baraza
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
      • Mwongozo wa Matumizi ya Vifaa vya TEHAMA
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Picha mwendo
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

MBEYA DC IMEAZIMISHA SIKU YA WAZEE DUNIAN

Imewekwa: October 1st, 2024

MAADHIMISHO SIKU YA WAZEE MBEYA DC

Na Fatina Msangi

Halmashauri ya wilaya ya Mbeya imeadhimisha siku ya wazee duniani kwa kuwakutanisha wazee kutoka maeneo mbalimbali wilayani humo ili kutafakari mchango wao katika Taifa na changamoto zinazowakabili.

Katibu wa baraza la wazee kata ya Inyala Jesko Linga akiwasilisha taarifa ya wazee hao ameishukuru Serikali kwa uimarishaji miundombinu mbalimbali ya wazee na kuomba kutatuliwa kwa baadhi ya kero zinazowakabili.

Baadhi ya kero hizo ni pamoja na uboreshaji madirisha ya wazee kwa kuhakikisha dawa zinapatikana hasa vijijini.

Akijibia suala hilo mwenyekiti wa Halmashauri ya Mbeya Mhe. Mwalingo Kisemba amesema dawa zinapatikana kwenye zahanati, vituo vya afya na hospitali mbalimbali kulingana na ukubwa wa eneo husika la utolewaji huduma.

"Hapa kwenye afya naomba mnisikilize Serikali inajitahidi kuleta dawa sema tofauti ni viwango, ukienda zahanati huwezipata kwenye kituo cha afya na ukienda kituo cha afya kuna dawa utazikosa hadi wilaya na baadaye hospitali ya rufaa ya mkoa na sisi tuna bahati hospitali ya wilaya iko hapahapa Inyala hadi kifaa kinaitwa Utra-sound kipo hapa kwa ajili ya kupima vitu vya ndani ya mwili bila kuingia ndani kwa hiyo mnaona namna gani Serikali imeboresha huduma za afya", amesema Mwalingo Kisemba.

Mwenyekiti wa Baraza la wazee wilaya ya Mbeya Filmon Nswila, ameomba agenda na maombi yao yatiliwe maanani na Serikali ili kufanyiwa maboresho hasa kwa kuthamini mchango wa wazee katika Taifa ambapo amesema mapendekezo yao yote wameyawasilisha kupitia maadhimisho ya kitaifa yaliyofanyika mkoani Tabora.

Kuhusu mapendekezo ya kuboreshwa na kuundwa kwa sheria za wazee, mgeni rasmi huyo ameeleza kupokea mapendekezo ya wazee wa wilaya ya Mbeya na kuahidi kumfikishia mbunge wa Mbeya vijijini Mhe. Oran Njeza ili kuona namna ya kufikisha juu mapendekezo yao ikiwa ni pamoja na kutungwa kwa sheria kadhaa juu ya kundi hilo muhimu katika jamii.

Oktoba mosi ya kila mwaka, Dunia huadhimisha siku ya Wazee, siku ambayo ilianzishwa na Baraza kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 14 Desemba 1990.

Maadhimisho haya ni sehemu ya utekelezaji wa mpango mkakati wa Vienna wa Mwaka 1982 kwa ajili ya wazee kote Duniani, “The Vienna International Plan of Action on Ageing” ulioboreshwa tena na mkakati wa Madrid, Hispania wa Mwaka 2002 ili kupambana na changamoto za wazee katika Karne ya 21 na kuendelea na mchakato wa maendeleo fungamani ya binadamu kwa ajili ya wote.

Kaulimbiu ya mwaka huu 2024 ni "TUIMARISHE HUDUMA KWA WAZEE WAZEEKE KWA HESHIMA".

Matangazo

  • VITUO VYA KUJIANDIKISHIA ORODHA YA WAPIGA KURA October 11, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA KUJITOLEA KWA KAZI YA MSAIDIZI WA WATOTO MAHAKAMANI February 02, 2022
  • TANGAZO LA ZOEZI LA UTOAJI WA ANWANIZA MAKAZI March 04, 2022
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA March 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MIKOPO SIO ZAWADI, NI YA MAENDELEO.

    July 03, 2025
  • DC MBEYA AFUATILIA AGIZO LA RC HOMERA UJENZI WA BARABARA YA MCHEPUKO IWAMBI MBALIZI, ARIDHISHWA NA KASI YAKE.

    June 10, 2025
  • Tuheshimu Sheria na taratibu zilizowekwa na Serikali- DED Erica..

    June 06, 2025
  • MbeyaDc yaadhimisha siku ya Mazingira Duniani kwa kufanya usafi katika Mto Mbalizi

    June 05, 2025
  • Tazama zote

Picha Mwendo

"Wapo Wakuu wa Idara na Vitengo wakiamishwa watu wanafanya sherere" Waitara Naibu waziri TAMISEMI
Picha mwendo zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MBEYA

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti ya mkoa wa Mbeya

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Mahali

Wasiliana nasi

    Mbaliz Road

    Sanduku la posta: 599

    Simu ya mezani: 025-2502260

    Simu ya mkononi: 0762210758

    Baruapepe: ded@mbeyadc.go.tz/info@mbeyadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma zetu

Copyright ©2018 Mbeya District Coucil . All rights reserved.