Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Bi. Erica Yegella ameyataka makundi maalum ya vijana na wanawake yaliyonufaika na mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri kuhakikisha fedha walizopata zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa, na si vinginevyo.

Mkurugenzi amesisitiza makundi nufaika kuwa mabalozi wazuri katika maeneo yao kwa kuonesha kwa vitendo namna Serikali ya Awamu ya Sita inavyowawezesha vijana, wanawake pamoja na watu wenye ulemavu kiuchumi.

“Msije mkafanya sherehe zisizo na tija kwa sababu mmeona mmepata fedha nyingi. Pelekeni fedha hizo kwenye biashara, mifugo na kilimo. Simamieni malengo mliyopanga ili baadaye tuone matunda ya mikopo mliyoipata. Hatutaki muishie kukopa milioni 50 tu; tunataka baadaye mfikie hata milioni 200,” amesisitiza Mkurugenzi Mtendaji huyo.

Hayo yamejiri leo wakati wa mafunzo kwa vikundi saba (7) vilivyonufaisha makundi ya vijana kwa kiasi kikubwa na wanawake, hatua inayoonesha dhamira ya Serikali katika kuimarisha uchumi wa wananchi kupitia uwezeshaji wa makundi maalum na kukuza sekta ya uzalishaji katika ngazi ya halmashauri.
Mbaliz Road
Sanduku la posta: 599
Simu ya mezani: 025-2502260
Simu ya mkononi: 0762210758
Baruapepe: ded@mbeyadc.go.tz/info@mbeyadc.go.tz
Copyright ©2018 Mbeya District Coucil . All rights reserved.