• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Mbeya District Council
Mbeya District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya Mbeya

  • Nyumbani
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mifugo na uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi
      • Ufugaji wa nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Wataalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
      • Taarifa ya fedha
      • Mpango wa Mapato na Matumizi
      • Mapato na Matumizi ya Mwezi
      • Taarifa ya miradi ya maendeleo
      • Taarifa ya fedha ya mwaka
      • Mihtasari ya Mikutano ya Baraza
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
      • Mwongozo wa Matumizi ya Vifaa vya TEHAMA
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Picha mwendo
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya afungia mgodi

Imewekwa: July 28th, 2017

Mkuu wa wilaya ya Mbeya, Mheshimiwa Paul Ntinika amefungia mgodi wa kuchimba madini aina ya mabowo uliopo kijijii cha Igalukwa kata ya Itawa. Mkuu wa Wilaya amefungia mgodi huo kwa kosa la kutofuata sheria na kanuni za uchimbaji wa madini nchini zinazomtaka mchimbaji kuwa na vibali kutoka Wizara ya Nishati na Madini, barua ya utambulisho kutoka ofisi ya madini kanda ikimtambulisha kwa Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya na Halmashauri ya Wilaya na Kijiji.

Mh. Ntinika amefungia mgodi huo alipofanya ziara ya kushtukiza akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi wa kijiji cha Igalukwa kuwa kuna watu wenye asili ya asia (wachina) wamevamia mashamba yao na kufanya shughuli za uchimbaji bila ya kuwa na taarifa yoyote.

“Tumepokea malalamiko toka kwa wananchi wa kijiji cha Igalukwa kata ya Itawa pamoja na Mheshimiwa diwani kuwa maeneo yao yamevamiwa na watu wasiokua na taarifa nao ambao wanachimba madini. Bahati nzuri tumefika hapa na tunaona mitambo mikubwa kweli na baadhi ya maeneo kuchimbwa na kuchongwa barabara. Na hata ukiangalia kwa macho tunashuhudia kuwa eneo hili limezungukwa na mashamba ya wananchi, sasa tumekuja ili kuona hawa watu wameingiaje katika eneo hili…”

Baada ya kuzungumza na wananchi Mh. Ntinika alizunguka kukagua mgodi huo na kugundua kuwa mgodi upo karibu na chanzo cha maji lakini waendeshaji wa mgodi huo hawajachukua hatua yoyote ya kukilinda chanzo hicho na badala yake wanatupia mabaki ya mawe na mchanga kwenye chanzo hicho hali inayohatarisha uhai wake. Baada ya kugundua uharibifu huo Mh. Ntinika aliwauliza watumishi wa mgodi huo na kukiri kuwa huo ni uharibifu unaofanywa na kampuni yao.

Kisha Mh. Ntinika alihitaji kuwaona wamiliki wa mradi huo lakini kwa bahati mbaya hawakuwepo mgodini hapo na wasimamizi waliokuwepo (wachina) hawakujua kuzungumza lugha ya Kiswahili wala Kiingereza, ndipo alipopewa namba ya mtu aliyefahamika kwa jina la Peter ambaye anafanya kazi katika mgodi huo kama msemaji wa kampuni. Baada ya kuwasiliana naye kwa simu Mh. Ntinika akatoa agizo la kufungia mgodi huo mpaka taratibu za kisheria zitakapokamilika.

Pia akifungia mgodi huo Mh. Ntinika ameagiza mawe ambayo yamechimbwa yasisafirishwe, wananchi kupitia Halmashauri ya Kijiji cha Igalukwa watasimamia ulinzi wa mgodi huo.

“Kama nilivyokuwa nawasiliana na msemaji wa kampuni ambaye anaongea lugha ya Kiswahili, kwa vile wenzetu hawajui lugha ya Kiingereza wala Kiswahili sasa uwaambie kwamba shughuli zote zinasimama mpaka watakapowasilisha taarifa yao kwa nini wamekiuka taratibu na hawajashirikisha kijiji, baada ya kupokea ndio tutatoa tamko lingine la shughuli kuendelea. Shughuli zote kuanzia leo zimesimama…. Wananchi wa eneo hili wataendelea kulinda, hakuna fujo itakayotokea hawa wakae kwa amani, wananchi nao wakae kwa amani. Mawe yasichukuliwe mpaka watakapo wasilisha taarifa”

Mheshimiwa Diwani wa Kata ya Itawa, Elia Mwampamba amemshukuru Mh. Ntinika kwa uamuzi aliochukua kwa kusema uamuzi huo unalenga kuleta ufumbuzi na suluhisho kwa wananchi ambao mashamba yao yameharibiwa

.“Ukweli uliopo ni kwamba kuna baadhi ya mashamba ya wananchi yameharibiwa hovyo bila kupewa fidia yoyote nipenda kuchukua nafasi hii kumshukuru Mku wa Wilaya baada ya kutoa agizo kwamba shughuli yoyote isiendelee hadi atakapokutana na uongozi wa kampuni hii kuangalia walikuje kujeje na kwa nini wameharibu mashamba ya watu na wananchi wanapata vipi fidia zao kwa wakati. Hivyo nishukuru sana kwa Mkuu wa Wilaya, naamaini wananchi haki yao wanaenda kuipata”

Matangazo

  • VITUO VYA KUJIANDIKISHIA ORODHA YA WAPIGA KURA October 11, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA KUJITOLEA KWA KAZI YA MSAIDIZI WA WATOTO MAHAKAMANI February 02, 2022
  • TANGAZO LA ZOEZI LA UTOAJI WA ANWANIZA MAKAZI March 04, 2022
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA March 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • KIAPO CHA UTII KWA WAUGUZI MBEYADC

    May 16, 2025
  • BI. ERICA AMEMTEMBELEA ASKALI ALIELAZWA HOSPITALI YA IFISI

    May 08, 2025
  • Mapokezi ya Mhe Mchengerwa MbeyaDc

    April 26, 2025
  • Karibu Mhe. Mchengerwa

    April 25, 2025
  • Tazama zote

Picha Mwendo

"Wapo Wakuu wa Idara na Vitengo wakiamishwa watu wanafanya sherere" Waitara Naibu waziri TAMISEMI
Picha mwendo zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MBEYA

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti ya mkoa wa Mbeya

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Mahali

Wasiliana nasi

    Mbaliz Road

    Sanduku la posta: 599

    Simu ya mezani: 025-2502260

    Simu ya mkononi: 0762210758

    Baruapepe: ded@mbeyadc.go.tz/info@mbeyadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma zetu

Copyright ©2018 Mbeya District Coucil . All rights reserved.