• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Mbeya District Council
Mbeya District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya Mbeya

  • Nyumbani
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mifugo na uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi
      • Ufugaji wa nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Wataalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
      • Taarifa ya fedha
      • Mpango wa Mapato na Matumizi
      • Mapato na Matumizi ya Mwezi
      • Taarifa ya miradi ya maendeleo
      • Taarifa ya fedha ya mwaka
      • Mihtasari ya Mikutano ya Baraza
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
      • Mwongozo wa Matumizi ya Vifaa vya TEHAMA
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Picha mwendo
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

RUZUKU YA MICHE YA KAHAWA YA SAMIA YAZIDI KUTIKISA MBEYA DC

Imewekwa: February 5th, 2026

Wakulima wa Kata ya Isuto, Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya (Mbeya DC), leo wamepatiwa bure jumla ya miche ya kahawa bora na ya kisasa 71,000, kupitia ruzuku ya asilimia 100 iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Sambamba na ugawaji wa miche hiyo, wakulima hao wamepatiwa pia elimu ya matumizi sahihi ya mbolea kwa ajili ya uzalishaji wa mazao mbalimbali, ikiwemo kahawa, ambayo ni miongoni mwa mazao muhimu ya biashara katika halmashauri hiyo.

Akizungumza wakati wa kukabidhi miche hiyo kwa wakulima wa vyama viwili vya ushirika; Chama cha Ushirika Shinzingo (Shinzingo AMCOS) na Chama cha Ushirika Umalila (Umalila AMCOS) kutoka vijiji vya Shizingo na Umalila mtawalia, Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Wilaya ya Mbeya, Cuthbert Mwinuka, amesema Serikali imeweka mkakati wa kutoa miche ya kahawa yenye ruzuku ili kuwawezesha wananchi kupata mbegu bora na za kisasa zitakazoongeza uzalishaji.

“Miche hii tuliyotoa leo ina uwezo mkubwa wa kuzalisha mazao mengi katika eneo dogo la ardhi, tofauti na mbegu za zamani. Mche mmoja unaweza kutoa mavuno ya wastani wa kilo moja (1) hadi kilo tano (5) za kahawa. Aidha, upandaji wake hauhitaji nafasi kubwa, hivyo katika hekari moja (1) mkulima anaweza kupanda hadi miche 1,000. Hii humwezesha mkulima kuvuna mazao mengi zaidi endapo atazingatia kanuni bora za kilimo,” amesema Mwinuka.

Kwa upande wake, Mtaalam wa Kilimo kutoka Kampuni ya Minjingu Mines and Fertiliser Limited, Juma Kayeke, amesema kampuni hiyo imeamua kushirikiana na halmashauri kuhakikisha wakulima wanapatiwa elimu ya matumizi sahihi ya mbolea kwa wakati muafaka, ili kusaidia ukuaji mzuri wa miche hiyo na kufanikisha uzalishaji uliokusudiwa.

“Sisi kama Minjingu Mines and Fertilizer Limited, tumekuwa tukizalisha mbolea kwa ajili ya mazao mbalimbali, ikiwemo kahawa. Leo tumetoa mbolea kwa vyama viwili vya ushirika katika kata hii kwa ajili ya mashamba ya mfano, ambayo yatasaidia wakulima kujifunza na kufanya maamuzi sahihi, ikiwemo matumizi ya mbolea zinazozalishwa na kampuni yetu,” amesema Kayeke.

Diwani wa Kata ya Isuto, Veronica Mzumbwe, ameishukuru Serikali kupitia halmashauri kwa jitihada kubwa ya kugawa miche ya kahawa kwa wananchi, akisema hatua hiyo itaongeza uzalishaji wa zao hilo kutokana na upatikanaji wa mbegu bora bure, kupitia ruzuku iliyowekezwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Naye Meneja wa Chama cha Ushirika Shizingo kutoka Kijiji cha Shizingo, Ntuta Mwozya, ameishukuru Serikali kwa kuwawezesha wakulima kupata miche ya kahawa bure pamoja na elimu ya matumizi ya mbolea, hatua itakayosaidia uzalishaji wa kahawa bora na yenye ubora wa juu zaidi.

Kwa upande mwingine, Mjumbe na Mwakilishi wa Chama cha Ushirika cha Umalila, Philemon Mwanijembe, amepongeza jitihada za Serikali katika kutoa ruzuku hiyo, akisema imeonesha dhahiri kujali maslahi ya wananchi wengi wanaotegemea kilimo kama chanzo kikuu cha maisha yao.

Matangazo

  • VITUO VYA KUJIANDIKISHIA ORODHA YA WAPIGA KURA October 11, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA KUJITOLEA KWA KAZI YA MSAIDIZI WA WATOTO MAHAKAMANI February 02, 2022
  • TANGAZO LA ZOEZI LA UTOAJI WA ANWANIZA MAKAZI March 04, 2022
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA March 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • RUZUKU YA MICHE YA KAHAWA YA SAMIA YAZIDI KUTIKISA MBEYA DC

    February 05, 2026
  • RUZUKU YA MICHE YA KAHAWA YA SAMIA YAZIDI KUTIKISA MBEYA DC

    February 05, 2026
  • DC ITUNDA AHIMIZA KUSIMAMIA MAPATO KWA MAENDELEO

    February 03, 2026
  • MBEYA DC YAPOKEA VIFAA KUWEZESHA MASIJALA MTANDAONI

    February 03, 2026
  • Tazama zote

Picha Mwendo

"Wapo Wakuu wa Idara na Vitengo wakiamishwa watu wanafanya sherere" Waitara Naibu waziri TAMISEMI
Picha mwendo zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MBEYA

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti ya mkoa wa Mbeya

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Mahali

Wasiliana nasi

    Mbaliz Road

    Sanduku la posta: 599

    Simu ya mezani: 025-2502260

    Simu ya mkononi: 0762210758

    Baruapepe: ded@mbeyadc.go.tz/info@mbeyadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma zetu

Copyright ©2018 Mbeya District Coucil . All rights reserved.