• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Mbeya District Council
Mbeya District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Mbeya District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Departments
      • Human Resources and Administration
      • Finance
      • Planning, Monitoring and Stastics
      • Health
      • Works
      • Water
      • Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Cleaning and Environment
      • Secondary Education
      • Agriculture, Irrigation and Cooperative
      • Primary Education
      • Land and Natural Resources
    • Units
      • ICT and Public Relations
      • Legal
      • Election
      • Internal Audit
      • Procurement Management
      • Bee keeping
  • Investment Opportunities
    • Tourists Attraction
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Expertise
  • Councilors
    • Councilors list
    • Standing Commitee
      • Finance, Administration and Planning Committee
      • Economics affairs, Construction and Environment Committee
      • Education, Health and Water Committee
      • AIDS Prevention Committee
    • Time table
      • Councilors Meetings
      • Visiting Chairperson
  • Projects
    • Approved Projects
    • On-going projects
    • Completed projects
  • Publications
    • By Laws
    • Service Contract
    • Strategic plan
    • Reports
      • Council Financial Report
      • Medium Term Expenditure Framework
      • Month Revenue and Expenditure Report
      • Council Development Report
      • Annual Performance and Financial Report
      • Full Council Minutes
    • Forms
    • Guidelines
      • Mwongozo wa Matumizi ya Vifaa vya TEHAMA
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery

Halmashauri Imezindua Mpango Mkakati wa Elimu wa Mwaka 2018

Posted on: October 31st, 2017

Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya imezindua mpango Mkakati wa elimu kwa shule za msingi wenye  lengo la kuinua ufaulu kutoka asilimia 61.4 ya mwaka 2017 hadi asilimia 93 kwa mwaka 2018. Akizindua mpango mkakati huo Katibu Tawala Wilaya ya Mbeya, Ndg, Hassan Mkwawa ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kwa kuzigeuza  changamoto zinazozikabili Idara ya Eliumu kuwa ni fursa na hatimaye kuja na mpango mkakati huo.

“Kumekuwa na changamoto nyingi ambapo wameamua changamoto hizo kuzigeuza kuwa malengo, na ni chukue fursa hii sasa kuwapongeza kwa sababu tungeendelea kuzichukulia hizi kama ni changamoto tusingekuja na mpango maalumu wa kuja kuinua kiwango cha ufaulu katika shule zetu”

Ndg. Mkwawa amesema kuwa ili malengo ya mkakati huo yaweze kufikiwa ni lazima Halmashauri iusimamie ipasavyo na kuhakikisha kila mdau anatekeleza majukumu yake ipasavyo.

Ndg. Mkwawa amezindua mpango mkakati huo kwenye kikao cha wadau wa elimu kilichoandaliwa na idara ya elimu msingi. Wadau waliohudhuria katika kikao hicho ni pamoja na wenyeviti wa vijij, watendaji wa vijiji, watedaji kata, waheshimiwa madiwani, walimu wakuu, maafisa elimu kata, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, wazazi, taasisi za fedha, taasisi za kiraia na wazazi.

Awali akiwasilisha mpango mkakati huo ili uweze kujadiliwa, Afisa Elimu Msingi Wilaya, Mwl. Vicent Kayombo amesema kuwa mpango mkakati huo unaitwa Mpango Mkakati wa Elimu wa Isuto wa mwaka 2018. Amesema umepewa jina la Isuto kwa sababu shule ya mwisho kiwilaya inatoka kata ya Isuto, na kuitaja shule hiyo kuwa ni Shule ya Msingi Shitete ambayo haikufaulisha hata mwanafunzi mmoja kati ya wanafunzi 36 waliofanya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi.

Pia Mwl. Kayombo amesema kuwa mpango mkakati huo umewasilishwa kwa wadau wa Halmashauri nzima ili waweze kuufahamu na kuwa na lengo moja kwani suala la ufaulu wa wanafunzi si suala la kuachiwa walimu pekeyao au idara ya elimu peke yake. Amesema kwa kutambua hilo ndio maana mpango mkakati huo umebeba kauli mbiu inayosema kuwa “Ufaulu wa Juu ni Ushirikiano wa Mimi na Wewe”

Vile vile amesema kuwa mpango mkakati huo umewasilishwa kwa wadau ili weweze kuujadili na kuuelewa kisha kuupeleka kwa wananchi kuutekeleza kwa pamoja, kwani wakiulewa wao kama viongozi itakuwa ni rahisi kutekelezwa.

“Leo sasa mpango huu, umeletwa mbele ya  wadau wa elimu, wadau wa elimu ambao  ni viongozi ili nao waweze kuupitia, kuachambua, ili maazimio yake, yatakuwa sasa ndio dira ya kushuka kule chini kwa wananchi. Idara ya Elimu Msingi inaamini kwamba wananchi wako tayari, wazazi wako tayari, tatizo ni sisi viongozi. Viongozi tukiwa na uelewa wa pamoja tukashusha maelekezo, tukawa mfano kule chini, tunaamini wazazi watatuunga mkoni kikamilifu, na hatimaye tutafikia malengo ambayo tumejiwekea.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri, Mhe. Ntokani akifunga mjadala baada ya wadau kuujadili na kuukubali mpango mkakati huo amesema kuwa kilichobaki sasa ni kufanya kwa vitendo. Na kuwaomba wadau kudumisha mshikamano na ushirikiano katika kutatua changamoto za elimu na kuzigeuza kuwa fursa kama mpango mkakati ulivyoelezea ili lengo liweze kufikiwa.

“naomba sana tujitahidi, baada ya kutoka hapa twende tukafanye kazi ya kushikana na kushikamana kwa kuhakikisha tunaziondoa hizo changamoto zilizopo kwenye maeneo yetu”

Announcements

  • VITUO VYA KUJIANDIKISHIA ORODHA YA WAPIGA KURA October 11, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA KUJITOLEA KWA KAZI YA MSAIDIZI WA WATOTO MAHAKAMANI February 02, 2022
  • TANGAZO LA ZOEZI LA UTOAJI WA ANWANIZA MAKAZI March 04, 2022
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA March 16, 2022
  • View All

Latest News

  • CRDB BENKI YATOA SHUKRANI KWA WATEJA WA HALMASHAURI

    September 17, 2025
  • RC MBEYA AHIMIZA MATUMIZI NISHATI SAFI.

    August 29, 2025
  • DC ITUNDA AKUTANA NA MACHIFU WA HALMASAHAURI YA WILAYA YA MBEYA

    August 28, 2025
  • DED ERICA E. YEGELLA APOKEA UGENI WA MACHIFU KUTOKA MKOA WA RUVUMA

    August 27, 2025
  • View All

Video

"Wapo Wakuu wa Idara na Vitengo wakiamishwa watu wanafanya sherere" Waitara Naibu waziri TAMISEMI
More Videos

Quick Links

  • MBEYA

Related Links

  • Ikulu
  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti ya mkoa wa Mbeya

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mbaliz Road

    Postal Address: 599

    Telephone: 025-2502260

    Mobile: 0762210758

    Email: ded@mbeyadc.go.tz/info@mbeyadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2018 Mbeya District Coucil . All rights reserved.