• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Mbeya District Council
Mbeya District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Mbeya District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Departments
      • Human Resources and Administration
      • Finance
      • Planning, Monitoring and Stastics
      • Health
      • Works
      • Water
      • Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Cleaning and Environment
      • Secondary Education
      • Agriculture, Irrigation and Cooperative
      • Primary Education
      • Land and Natural Resources
    • Units
      • ICT and Public Relations
      • Legal
      • Election
      • Internal Audit
      • Procurement Management
      • Bee keeping
  • Investment Opportunities
    • Tourists Attraction
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Expertise
  • Councilors
    • Councilors list
    • Standing Commitee
      • Finance, Administration and Planning Committee
      • Economics affairs, Construction and Environment Committee
      • Education, Health and Water Committee
      • AIDS Prevention Committee
    • Time table
      • Councilors Meetings
      • Visiting Chairperson
  • Projects
    • Approved Projects
    • On-going projects
    • Completed projects
  • Publications
    • By Laws
    • Service Contract
    • Strategic plan
    • Reports
      • Council Financial Report
      • Medium Term Expenditure Framework
      • Month Revenue and Expenditure Report
      • Council Development Report
      • Annual Performance and Financial Report
      • Full Council Minutes
    • Forms
    • Guidelines
      • Mwongozo wa Matumizi ya Vifaa vya TEHAMA
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery

Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Imetoa mkopo wa Milioni 174 kwa vikundi 46 vya Wanawake na Vijana

Posted on: October 6th, 2017

Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya imetoa mkopo wa Shilingi Milioni 174 kwa vikundi 46 vya wanawake na vijana. Kati ya vikundi hivyo vilivyopata mkopo vikundi 31 ni vya wanawake ambavyo vimepata mkopo wenye thamani ya Shilingi Milioni 121, na vikundi 15 ni vya vijana vilivyopatiwa mkopo wa Shilingi Milioni 53.

Akikabidhi mkopo huo kwa walengwa Mkuu wa Wilaya ya  Mbeya, Mhe. Willium Paul Ntinika ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kwa kutekeleza agizo la Serikali linalozitaka Halmashauri zote nchini kutenga asilimia kumi (10%) ya mapato yake kila mwaka kwa ajili ya kutoa mikopo kwa wanawake na vijana.

“Nitoe shukurani zangu za dhati kuipongeza Halmashauri, nimpongeze Mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na Mkurugenzi Mtendaji kwa kuendelea kutekeleza agizo la serikali, hongereni sana”

Pia Mhe. Ntinika amewataka wanavikundi waliopata mikopo hiyo kuitumia kwa tija ili lengo lililowekwa na Serikali katika kutoa mikopo hiyo liweze kufukiwa. Mhe. Ntinika amesema mikopo waliyopewa si zawadi bali wamepewa kwa ajili ya kujiendeleza kiuchumi na watalazimika kuirejesha baada ya kuisha siku thelathini ili wananchi wengine waliokosa mikopo hiyo awamu hii waweze kupata katika awamu zinazofuata.

 “Pia naomba kuchukua fursa hii kuwapongeza wanavikundi mliobahatika kupata mikopo hii kwa siku hii ya leo kwa sababu nina amini kuna wengi waliomba lakini nyie mpata bahati hii kwa hiyo bahati hii muitumieni vizuri. Nina amini mikopo hii inayokuja kwenu itafanye kazi iliyokusudiwa kwa sababu mmeandika kusudio la kuomba mkopo,  mkopo huo uende sambamba na kile ambacho mlichokusidia, laniki mkumbuke kurejesha. Nilifundisha mwaka jana kwamba ukipewa mkopo pige hesabu yako kwaba kila mwezi unatakiwa kurudisha shilingi ngapi, unaziandika muda ukifika unarudisha. Hivyo basi matarajio yangu ni kwamba mikopo hii mtaanza kurejesha baada ya kuisha siku 30”

Licha ya kuwasisitiza wanavikundi kurejesha pesa walizokopa kwa wakati, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Mhe. Kisemba Mwalingo amewataka wanavikundi hao kuwa wabunifu katika kufanya kazi zao ili kufikia uchumi wa viwanda kwa kuanzisha viwanda vidogo ili kumuunga mkono Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa kauli mbiu yakwe inayosema Tanzania ya viwanda.

“kwa bahati mbaya sana Rais anaposema Tanzania ya Viwanda watu wandani hii ni ndoto isiyotekelezeka kwa sababu hawajui ni ni maana ya kiwanda, hawajui kwamba kunaviwanda vikubwa, vya kati na vidogo. Naomba muelewe kwamba kiwanda ni kubadilisha malighafi kwenda katika kutumika.  Kwamba kama ilikua pamba izae nguo, kama yalikua maembe yazae juisi. kinachofanya hivyo ni kiwanda sasa maana yangu ni nini? Maana yangu ni kwamba akinamama tunaviwanda lakini hatuvijui, kwa maana ya kuelewa neno kiwanda kila nyumba inayopika mboga na ugali ni kiwanda kwa sababu inabadilisha unga kuwa ugali”

“Kwa hiyo tunaposema kiwanda tusiwe tukafikiri ni jambo pana sana, ni jambo kubwa sana. akija mzungu hapa akapika maharage kwenye jiko, na akayaweka kwenye kopo tunasema hiki ni kiwanda lakini hakija huyu mama akipika maharage akayaweka kwenye sahani mkala hakiwi kiwanda. Kwa hiyo viwanda mnatembea navyo kazi ni kuviboresha tu, tuwe wabunifu viwe vizuri ili vipate soko.”

Awali akisoma risala kawa mgeni rasmi, Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Ndg. Zena Kapama amesema kuwa, Halmashauri imeweka mkakati wa kutoa mikopo kutokana na pesa zamakusanyo ya ndani kila robo baada ya kutoa mara moja kwa mwaka kama iliyokuwa awali.

“Mhe. Mgeni rasmi katika kutekeleza azma ya Serikali ya kufikia maendeleo endelevu na malengo ya pamoja, pamoja na mkakati wa nchi yetu wa Serikali ya viwanda. Mkakati wetu Mhe. Mgeni rasmi ni kwamba kila robo tutakuwa tunatoa mikopo kwa kupitia fedha yetu ya makusanyo ya ndani kwa wanawake na vijana”

 

Announcements

  • VITUO VYA KUJIANDIKISHIA ORODHA YA WAPIGA KURA October 11, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA KUJITOLEA KWA KAZI YA MSAIDIZI WA WATOTO MAHAKAMANI February 02, 2022
  • TANGAZO LA ZOEZI LA UTOAJI WA ANWANIZA MAKAZI March 04, 2022
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA March 16, 2022
  • View All

Latest News

  • CRDB BENKI YATOA SHUKRANI KWA WATEJA WA HALMASHAURI

    September 17, 2025
  • RC MBEYA AHIMIZA MATUMIZI NISHATI SAFI.

    August 29, 2025
  • DC ITUNDA AKUTANA NA MACHIFU WA HALMASAHAURI YA WILAYA YA MBEYA

    August 28, 2025
  • DED ERICA E. YEGELLA APOKEA UGENI WA MACHIFU KUTOKA MKOA WA RUVUMA

    August 27, 2025
  • View All

Video

"Wapo Wakuu wa Idara na Vitengo wakiamishwa watu wanafanya sherere" Waitara Naibu waziri TAMISEMI
More Videos

Quick Links

  • MBEYA

Related Links

  • Ikulu
  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti ya mkoa wa Mbeya

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mbaliz Road

    Postal Address: 599

    Telephone: 025-2502260

    Mobile: 0762210758

    Email: ded@mbeyadc.go.tz/info@mbeyadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2018 Mbeya District Coucil . All rights reserved.