• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Mbeya District Council
Mbeya District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Mbeya District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Departments
      • Human Resources and Administration
      • Finance
      • Planning, Monitoring and Stastics
      • Health
      • Works
      • Water
      • Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Cleaning and Environment
      • Secondary Education
      • Agriculture, Irrigation and Cooperative
      • Primary Education
      • Land and Natural Resources
    • Units
      • ICT and Public Relations
      • Legal
      • Election
      • Internal Audit
      • Procurement Management
      • Bee keeping
  • Investment Opportunities
    • Tourists Attraction
    • Agriculture
    • Livestock
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Expertise
  • Councilors
    • Councilors list
    • Standing Commitee
      • Finance, Administration and Planning Committee
      • Economics affairs, Construction and Environment Committee
      • Education, Health and Water Committee
      • AIDS Prevention Committee
    • Time table
      • Councilors Meetings
      • Visiting Chairperson
  • Projects
    • Approved Projects
    • On-going projects
    • Completed projects
  • Publications
    • By Laws
    • Service Contract
    • Strategic plan
    • Reports
      • Council Financial Report
      • Medium Term Expenditure Framework
      • Month Revenue and Expenditure Report
      • Council Development Report
      • Annual Performance and Financial Report
      • Full Council Minutes
    • Forms
    • Guidelines
      • Mwongozo wa Matumizi ya Vifaa vya TEHAMA
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery

Ndg. Juma Makelele achaguliwa tena kuwa Makamu Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mjii Mdogo wa Mbalizi

Posted on: October 19th, 2017

Wajumbe wa Mamlaka ya Mji mdogo wa Mbalizi wamemchagua tena Ndg Juma Makelele Kuwa Makamu Mwenyekiti wa Mamlaka hiyo.kwa awamu nyingine ya mwaka wa fedha 2017/2018. Afisa Tawala Wilaya Ndg. Amimu Mwandelile amemtangaza Mhe. Juma Makelele kuwa Makamu Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbalizi kwa kupata kura tisa dhidi ya kura saba alizozipata Ndg Diphasi Mwakisale Kwenye Mkutano wa uchaguzi wa kumchagua Makamu Mwenyekiti na kuunda kamati za kudumu za Mamlka ya Mji Mdogo Mbalizi.

Kabla ya kutangaza matokeo Ndg. Mwandelile aliwaeleza wajumbe kuwa kwa mujibu wa Sheria, taratibu na kanuni zinazosimamia Mamlaka za Serikali za Mitaa ni kwamba Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mjimdogo anadumuu madarakani kwa muda wa miaka mitano lakini makamu wake anachaguliwa kila baada ya mwaka mmoja. Baada ya kusema hivyo akampa nafasi aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Mamlaka hiyo Ndg. Juma Makelele kujiuzuru nafasi yake kabla ya kugombea tena, kisha uchauzi ukaanyika na kumtangaza Ndg. Juma Makelele ameshinda tena nafasi hiyo.

“kura zilizopigwa zilikua ni 16, hakuna kura iliyoharibika, kasoro mjumbe mmoja tu hakuudhuria, nataja kura zilizopatikana, Ndg. Diphasi Mwakisale amepata kura saba, Ndg. Juma Makelele amepata kura tisa. Kwa hiyo kwa mamlaka niliyopewa kama msimamizi wa uchaguzi namtangaza rasmi Juma Makelele kuwa Makamu Mwenyekiti wa Mji Mdogo wa Mbalizi”

Akitoa shukurani zake kwa wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo Mbalizi, Ndg. Makelele amesema kuwa sasa ni wakati wa kazi, uchaguzi ushaisha nay eye binafsi anahesabu kuwa wajumbe wote walimchagua yeye hivyo kwake hakutakuwa na tofauti yoyote. Pia aliwaomba wajumbe wasisite kumkosoa na kumshauri pale atakapokosea kwa lengo la kuijenga mamlaka hiyo.

“Ndg wajumbe nipende tu kuwashukuru kwa kazi nzuri mliyoifanya nawashukuru sana, wale walioweza kunipa kura na ambao hawajanipa nasema kwamba wote wamenipa. Nawashukuru sana naoma ushirikiano tuzidi kusonga mbele., Pale kwenye mapungufu naomba niambiwe, hakuna mtu ambaye hakusolewi wakati kunaonekana kunatatizo. Ili tufanye kazi tuimizane weto wajumbe tupo kitu kimoja, pale tunapokosea tuambizane, tusonge mbele ili mamlaka yetu isonge mbele, nawashukuru sana, asanteni sana”

Baada ya kumchagua Makamu Mwenyekiti, Mtendaji wa Mamlaka ya Mji mdogo wa Mbalizi, Ndg. Kassimu Ugulumo aliwatangazia wajumbe kuwa hatua inayofuata ni kuunda kamati za kudumu,ambazo ni; Kamati ya Elimu, Afya na Maji, Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira, Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango Miji. Alisema kwa mujibu wa kanuni kamati hizo zinaundwa kwa Mwenyekiti wa Mamlaka kupendekeza majina ya wajumbe na kisha majina hayo kujadiliwa na kupitishwa na Mamlaka. Hivyo kama kunamapendekezo yoyote wanapenda kuyawasilisha kanuni zinawaruhusu.

 

Kisha akaongeza kwamba baada ya kupitisha kila kamati itamchagua mwenyekiti wa kamati yake ambaye kwa mujibu wa kanuni ataingia moja kwa moja kwenye kamati ya Fedha, Utawala na Mipango Miji wakiungana na wajumbe wanaoingia kwa nafasi zao; yaani Mwenyekiti wa Mamlaka, Makamu Mwenyekiti pamoja na Mhe. Mbunge pamoja na wengine wanaopendekezwa na Mwenyekiti wa Mamlaka.

 “hatua inayofuata ni kuunda kamati za kudumu, kwa kanuni zilizopo Mwenyekiti anatoa mapendekezo, lakini hayo mapendekezo yanaweza kujadiliwa lakini kama yanaafikiwa yanapita kama yalivyo, na ntakapowataja hawa waliopendekezwa watatoka nje watachaguana mwenyekiti, kila kundi litachagua mwenyekiti.wake. Wale wenyeviti ndio watakaokuwa wajumbe moja kwa moja wa Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango Miji… mwenyekiti anamamlaka ya kuwateua wengine kuingia moja kwa moja kwenye Kamati ya Fedha.”

 

  

Baada ya zoezi hilo kukamilikwa kwa amani na utulivu Mbunge wa jimbo la Mbeya Vijijini Mhe. Oran Njeza aliwapongeza wajumbe wote kwa hatua nzuri waliyofikia na kuwataka waongeze mshikamano katika mambo ya kimaendeleo ili kuiwezesha Mamlaka hiyo kukidhi vigezo vya kuwa Halmashauri ya Mji.

“Nianze kwa kushukuru tena kushukuru sana kwa hili zoezi la uchaguzi kuisha vizuri. Mbeya Vijijini kwa kweli kwa ujumla hasa Mbalizi nafikiri tunakwenda vizuri na nafikiri twende vizuri hivyo hivyo. Sasa naomba katika kipindi hiki kilichobaki tuwe na msimamo huo ili tuione Mbalizi yetu tuiletee mabadiliko. Katika kipindi hiki sisi ndio viongozi wa Serikali ya Mji Mdogo wa Mbalizi tukisaidiana na wataalamu wetu. Ndugu zangu tunamajukumu makubwa sana, na wananchi wanamategemeo makubwa mno, kwa hiyo naomba sana tena sana hizi kamati zilizoundwa tusione hiki kitu ni cha Diwani, Hiki kitu ni cha Mbunge hiki kitu ni cha Serikali kuu. Kwenye eneo lako uliko kitu cha maendeleo ni cha kwako”

Announcements

  • VITUO VYA KUJIANDIKISHIA ORODHA YA WAPIGA KURA October 11, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA KUJITOLEA KWA KAZI YA MSAIDIZI WA WATOTO MAHAKAMANI February 02, 2022
  • TANGAZO LA ZOEZI LA UTOAJI WA ANWANIZA MAKAZI March 04, 2022
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA March 16, 2022
  • View All

Latest News

  • CRDB BENKI YATOA SHUKRANI KWA WATEJA WA HALMASHAURI

    September 17, 2025
  • RC MBEYA AHIMIZA MATUMIZI NISHATI SAFI.

    August 29, 2025
  • DC ITUNDA AKUTANA NA MACHIFU WA HALMASAHAURI YA WILAYA YA MBEYA

    August 28, 2025
  • DED ERICA E. YEGELLA APOKEA UGENI WA MACHIFU KUTOKA MKOA WA RUVUMA

    August 27, 2025
  • View All

Video

"Wapo Wakuu wa Idara na Vitengo wakiamishwa watu wanafanya sherere" Waitara Naibu waziri TAMISEMI
More Videos

Quick Links

  • MBEYA

Related Links

  • Ikulu
  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti ya mkoa wa Mbeya

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mbaliz Road

    Postal Address: 599

    Telephone: 025-2502260

    Mobile: 0762210758

    Email: ded@mbeyadc.go.tz/info@mbeyadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2018 Mbeya District Coucil . All rights reserved.