• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Mbeya District Council
Mbeya District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya Mbeya

  • Nyumbani
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mifugo na uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi
      • Ufugaji wa nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Wataalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
      • Taarifa ya fedha
      • Mpango wa Mapato na Matumizi
      • Mapato na Matumizi ya Mwezi
      • Taarifa ya miradi ya maendeleo
      • Taarifa ya fedha ya mwaka
      • Mihtasari ya Mikutano ya Baraza
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
      • Mwongozo wa Matumizi ya Vifaa vya TEHAMA
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Picha mwendo
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

MBEYA DC YASAJILI 483 BIMA YA AFYA KWA WOTE

Imewekwa: February 13th, 2026

Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya (Mbeya DC) imesajili jumla ya wananchi 483 katika Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, kutoka kundi la wananchi wasio na uwezo wakiwemo wazee, watoto na wajawazito. Wananchi hao wanagharamiwa moja kwa moja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Taarifa hiyo imetolewa leo na Afisa Uanachama Mwandamizi kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), kwa niaba ya Meneja wa NHIF Mkoa wa Mbeya, Calistus Mpangala, wakati wa Kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mbeya DC kilichoketi kujadili na kupitisha Rasimu ya Mapendekezo ya Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027.

Akizungumza katika kikao hicho, Mpangala amesema NHIF inaendelea na zoezi la usajili wa wananchi kutoka kaya masikini, ikiwemo zile zinazotambuliwa na Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF). Amesema zoezi hilo ni sehemu ya utekelezaji wa maono na ahadi ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, aliyoitoa wakati wa kampeni za uchaguzi wa mwaka 2025, ya kutekeleza mpango huo ndani ya siku 100 endapo angechaguliwa.

“Naomba niwasihi Waheshimiwa Madiwani kuendelea kuhamasisha kaya zote zilizo katika mpango wa TASAF kwenye maeneo yao zijitokeze kwa ajili ya usajili, ili tuweze kutekeleza kikamilifu azma hii kama ilivyoelekezwa na Mheshimiwa Rais,” amesisitiza Afisa Uanachama Mwandamizi wa NHIF.

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa, Mbeya DC ina jumla ya wananchi 3,944 wanaotoka katika kaya masikini. Hadi sasa, wananchi 483 tayari wameshasajiliwa katika Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, huku zoezi likiendelea katika kata za Igonza, Ulenje na Ilungu, kwa lengo la kuhakikisha agizo la Mheshimiwa Rais linatekelezwa kwa ufanisi.

Aidha, Mpangala amebainisha kuwa kitaifa, Tanzania inakadiriwa kuwa na zaidi ya kaya masikini milioni 3.7. Hata hivyo, kaya zinazotambulika rasmi hazizidi 900,000. Katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, Serikali imefanikiwa kugharamia usajili wa kaya takribani 278,000.

Matangazo

  • VITUO VYA KUJIANDIKISHIA ORODHA YA WAPIGA KURA October 11, 2024
  • TANGAZO LA KAZI YA KUJITOLEA KWA KAZI YA MSAIDIZI WA WATOTO MAHAKAMANI February 02, 2022
  • TANGAZO LA ZOEZI LA UTOAJI WA ANWANIZA MAKAZI March 04, 2022
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA March 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MBEYA DC YASAJILI 483 BIMA YA AFYA KWA WOTE

    February 13, 2026
  • MWENYEKITI MBEYA DC AKABIDHI VISHIKWAMBI 44 KWA MADIWANI KUIMARISHA UFANISI WA KAZI

    February 13, 2026
  • MKURUGENZI, WATENDAJI VIJIJI MBEYA DC WAJADILI MIKAKATI KUHARAKISHA MAENDELEO

    February 12, 2026
  • MBEYA DC YASISITIZA MATUMIZI SAHIHI MIKOPO YA ASILIMIA 10

    February 11, 2026
  • Tazama zote

Picha Mwendo

"Wapo Wakuu wa Idara na Vitengo wakiamishwa watu wanafanya sherere" Waitara Naibu waziri TAMISEMI
Picha mwendo zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MBEYA

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti ya mkoa wa Mbeya

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Mahali

Wasiliana nasi

    Mbaliz Road

    Sanduku la posta: 599

    Simu ya mezani: 025-2502260

    Simu ya mkononi: 0762210758

    Baruapepe: ded@mbeyadc.go.tz/info@mbeyadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma zetu

Copyright ©2018 Mbeya District Coucil . All rights reserved.