Mkurugenzi Mtendaji Bi Erica E Yegella amewataka waendesha vyombo vya moto barabarani kutii sheria zilizowekwa ili kuepusha ugomvi na kugoma kunakowasababishia wananchi wanakosa Usafiri.
Bi Erica ameyasema hayo leo Mei 29, 2025 alipokutana na kufanya kikao na viongozi wa Bajaji na Daladala ili kutatua mgogoro wao ulodumu kwa muda wa miezi miwili sasa, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa halmashauri.
"Kila sehemu kuna sheria na taratibu zake hata barabarani kunautaratibu wake, sheria ipo wazi kwa upande wa bajaji na daladala pamoja na mipaka ili tusiingiliane" alisema Bi Erica
Aidha Mkurugenzi ameongezea kuwa ili kuondoa mgogoro ndani ya siku tatu kutawekwa vibao vya kuonesha sehemu zote wanazotakiwa bajaji kuegesha ili kuondoa mgogoro.
Pia amewataka kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi kwani tabia hizi zitapelekea kukamatwa na kuwekwa ndani.
Kikao hicho kimehudhuriwa na OCD MM.Mrema, Eng. Hamis kutoka LATRA, TEO Mbembela, Afisa biashara Bi Anitha Mdee na Afisa Mapato Bwana Kivisa.
Mbaliz Road
Sanduku la posta: 599
Simu ya mezani: 025-2502260
Simu ya mkononi: 0762210758
Baruapepe: ded@mbeyadc.go.tz/info@mbeyadc.go.tz
Copyright ©2018 Mbeya District Coucil . All rights reserved.