Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Bi Erica E Yegella amewataka wananchi wa kitongoji cha Idugumbi kilichopo Kata ya Utengule Usongwe kufuata sheria na taratibu zilizowekwa na Serikali na kuheshimu mamlaka inayowaongoza.
Bi Erica ameyasema hayo leo Juni 6, 2025 alipofanya mkutano wa hadhara katika kitongoji hicho.
Amesema Serikali haitafumbia macho wanaokusanya mapato bila utaratibu ulowekwa na Serikali akiongea na wananchi wa kitongoji hicho amesititiza ukusanyaji wa mapato utumie "Pos au control namba" zinazotolewa na Halmashauri kupitia Maafisa mapato.
Mkurugenzi amesisitiza kuwa wale wote wenye fedha mkononi waende kwa afisa mapato ambaye alikuwepo kwenye mkutano huo ili waziwasilishe kwa control namba kabla Halmashauri haijatumia nguvu.
Aidha wananchi wa kitongoji hicho wamemshukuru Mkurugenzi kwa kufika na kuitikia wito wa kuja kuwasikiliza kero zao, ikiwa kero kubwa ni umaliziaji wa ujenzi wa Zahanati ya Idugumbi ambao umesimama kwa muda sasa.
Bi Erica amesema kuhusu Zahanati atamtuma mhandisi kufika hapo na kufanya tathimini ili Halmashauri imalizie ujenzi huo ambao wananchi walianzisha.
Mkurugenzi mtendaji amewashukuru wananchi wa Idugumbi kwa kuitikia wito na kuwa wawazi. Ameongeza pia swala lao la ubadhilifu wa matumizi ya fedha kwenye ujenzi wa Zahanati hiyo tayari yapo TAKUKURU yanafanyiwa kazi.
@ortamisemi
@mohamed_mchengerwa @benomalisa @juma_zuberi_homera
Mbaliz Road
Sanduku la posta: 599
Simu ya mezani: 025-2502260
Simu ya mkononi: 0762210758
Baruapepe: ded@mbeyadc.go.tz/info@mbeyadc.go.tz
Copyright ©2018 Mbeya District Coucil . All rights reserved.